Thursday 3 September 2015

USHAURI KWA NATUMIZI YA MTANDAO

SOMA

ninachoamini watu wote wanaotumia social media kama hii, wana uwezo wa kusoma na kuandika kama wewe ulivyo. hebu jaribu kusoma hapa inaweza ikakusaidia kwa namna moja au nyingine! umewahi kujiuliza, kuna utofauti gani kati ya maisha ya watu walioishi zamani miaka hamsini iliyopita na sisi ambao tunaishi leo? nadhani utakubaliana na mimi kuwa watu wa kale walikuwa hawajui mambo mengi kama ilivyo leo hii. leo watu wanafahamu mambo yao pamoja na mambo ya wengine tena mbaaali kabisa. kwa mafano unaweza ukawa unajua mila za kwenu na mila za kabila jingine kwa kujifunza kupitia mtandaoni tuu. Hii yote ni kwa ajili ya kukua kwa sayansí ya teknolojia mawasiliano pamoja na uhuru wa vyombo vya habari. Walahi tungejua matumiz mazur ya sayansi hii Kizazi cha leo tungekuwa innovative kuliko hata akina newton, eistein na wengine unaowafahamu.. lakini tumekuwa na matumiz mabaya ya mtandao kwa kupotezeana muda kwa kushirikisha mambo yasiyo na maana tukijisahau kuwa tuna wajibu wa kuandika historia za maisha yetu kabla hatujafa. Embu kijana funguka, ukiunga bando lako epuka suffing za vitu visivyo na tija kwako. chukua vile vinavyokuhusu. kama ni mwanasiasa fuatilia mambo ya siasa, mwanauchumi na uchumi, mwanateknolojia na teknolojia, mwanahabari na habari za kujenga. tuache kulike page zisizo na maana na zinazotufanya tusahau utu wetu, epuka kushirikisha mambo yanayopotosha jamii na yanayojenga upotevu wa amani. TUMIA MTANDAO KWA KUJIFUNZIA, UTAONA FAIDA YAKE.
Asante kwa kusoma.

by Materu Godlove


information securty specialist

0 maoni:

Post a Comment